Klabu ya Dar es Salaam Young Africans leo June 1 2016 kupitia katibu mkuu wakeBaraka Deusdedit wametoa kalenda ya uchaguzi mkuu wa klabu hiyo, ikiwa ni siku chache zimepita toka shirikisho la soka Tanzania litangaze kuwa uchaguzi wa Yangautafanyika ndani ya siku 60ila Yanga wametangaza 11/06/2016.
Bado kuna mvutano kati ya TFF na Yanga, ukweli ni kuwa Yanga hawataki uchaguzi wao usimamiwe na kamati ya uchaguzi wa TFF “Serikali
iliagiza uchaguzi wa Yanga ufanyike hadi June 30 lakini baadae TFF
wakatangaza tarehe yao, kwa kifupi uchaguzi wa Yanga utasimamiwa na
kamati ya usajili ya Yanga, Yanga sio footbal club ni sports club”
Hakuna maoni:
Write maoni