MJUE MWANDISHI NA KALAMU YAKE
Habari za wakati huu wapenzi wa riwaya... Naam, nakukaribisheni
kwenye makala yetu hii ya 'MJUE MWANDISHI NA KALAMU YAKE' ninae kuletea
makala hii ni mimi Zubery Razuur Mavugo.
MAKALA Leo katika makala yetu tutayatazamia maisha ya Mwandishi kwa jina la HASSAN OMARI MAMBOSASA.
HISTORIA YA MAISHA YAKE KIUFUPI
Jina lake kamili anaitwa Hassan Omari Mambosasa, ni mzaliwa wa nne
katika familia ya mzee Omari, lakini pia ni mzaliwa wa kwanza upande wa
Mama yake kipenzi Bi. Swaumu Mohamed Suleiman. Amezaliwa tarehe 14
februali mwaka 1993 katika Hospitali ya Ngamiani huko Tanga. Alianza
kusoma elimu yake ya msingi mnamo mwaka 1999 katika shule ya msingi
Koboko. Kutokana na kurudishwa darasa la kwanza kwa mara ya pili
kulimpelekea ahitimu darasa la saba mwaka 2006 katika shule ya msingi
Kizuiani iliyopo Mbagala.
Elimu ya sekondari kidato cha kwanza hadi
cha nne amepitia shule tatu tofauti, ambazo ni ; Jitegemee, Ubungo
islamic na Wailesi kitendo kilichomfanya akariri kidato cha pili
kutokana na kuhamishwa shule moja kwenda nyingine. Alihitimu kidato cha
nne mwaka 2011.
‘’Nilianza kidato cha tano shule ya sekondari
Tambaza hadi nilipohitimu mwaka 2014 kisha nikajiunga na Jeshi la
kujenga Taifa kwa mafunzo mafupi.’’ Mambosasa alisema.
Mambosasa
mpaka sasa ana elimu ya kidato cha sita ambayo tayari amesha ikamilisha,
lakini pia bado anasoma, yupo Chuo. Anasomea ‘Computer Science’ huko
Songea, ndani ya chuo kijulikanacho kwa jina la ST. Joseph.
NDOTO ZA KUWA MTUNZI WA MAANDISHI
Ndoto za kuandika zilimjia punde tu baada ya kumuona rafiki yake
kipenzi [hatujafanikiwa kulitambua jina lake kwakuwa makala yetu ni
mbegu] ambaye alikuwa mchoraji mwenzake; rafiki yake huyo alikuwa
akipenda kuchora kisha anaandika maandishi kwenye mchoro aliyo uchora,
kitendo kilichomvutia sana Hassan na hapo ndipo aliposhawishika kwa
kiasi kikubwa kuandika, ingawa alikuwa akichukulia kama sehemu yake ya
kujifurahisha tu. Lakini siku nenda siku rudi ndipo alipokuja kugundua
kipaji chake.
HADITHI YAKE YA KWANZA.
Hassani Mambosasa ingawa alikuwa akipenda kuandika lakini hakuwa amewahi
kuandika hadithi nzima japokuwa kila siku, saa na hata dakika hadithi
zilikuwa zikijitunga kichwani mwake.
‘’Hadithi yangu ya kwanza
ilikuwa ikiitwa JOKA LA AJABU niliiandika kwenye karatasi ambazo
nilizikunja mara mbili zikawa zipo kwenye mfumo wa kitabu.’’ Mambosasa
alisema siku moja baada ya kutembelewa na mmoja kati ya watoa habari
wetu wa kutoka hapahapa Becker tv
KUJIINGIZA, MTANDAONI.
Hassani Mambosasa anasema kuwa, alijiingiza mtandaoni akiwa kama mtu
wa kawaida tu aliyetaka kuwasiliana na watu mbalimbali pamoja na kupata
marafiki wapya. Akiwa kwenye pitapita zake hapa na pale ndipo
alipokutana na ukurasa ambao hapo zamani ulijulikana kwa jina la Kona ya
Riwaya ingawa hivi sasa unajulikana kwa jina la Kona ya Riwaya
‘reloaded’, huko ndiko alikoshawishika na yeye kuandika riwaya mtandaoni
kwa mara ya kwanza kabisa. Hadithi yake ya kwanza kuiandika mtandaoni
ilijulikana kwa jina la SADAKA na hiyo ni baada ya kupata ushawishi na
hamasa kutoka kwenye ukurasa wa kona ya riwaya.
CHANGAMOTO.
‘’Changamoto nilizopitia ni nyingi sana lakini muda pamoja na ukosefu
wa kitendea kazi hapo kipindi cha nyuma ndivyo vilinisumbua sana’’
Hassani alisema baada ya kuhojiwa na mwandishi wetu wa makala ya mjue
mwandishi na kalamu yake
MAFANIKIO.
‘’Mafanikio
sina makubwa sana kiasi cha kuweza kuyatangaza lakini napenda niseme tu
kupitia uandishi nimejikuta nikisogea kwenye hatua moja nzuri sana.’’
Mambosasa alisema.
ANACHOSEMA KWA MASHABIKI ZAKE.
'’Ninachowaambia mashabiki zangu ni kwamba, waendelee kuwa nami kwani
kuna vizuri vinakuja zaidi ya wanavyovisoma, lakini pia naomba wazidi
kunipatia sapoti yao kwani hakuna fanani bila hadhira hata siku moja.’’
Alisema.
BAADHI YA KAZI ZAKE NI;
NSUNGI.
WAKALA WA GIZA.
WITO WA KUZIMU.
SHUJAA.
SHUHUDA.
KOSA.
DHAHAMA.
JINAMIZI.
NA NYINGINEZO NYINGI......
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Write maoni