Jumatano, 15 Juni 2016

Beyonce achangisha $82k kusaidia mradi wa maji Marekani

Beyonce amechangisha dola 82,234 kwaajili ya kusaidia wakazi wa eneo la Flint, Michigan nchini Marekani wanaokabiliwa na tatizo kubwa la maji.

Kwa mujibu wa Detroit Free Press, Queen Bey amekusanya kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kuwasaidia wakazi wa kitongoji cha Flint ambao wameteseka kwa muda mrefu kutokana na mgogoro uliopo. Pia Beyonce amewasaidia kuwalipia ada ya shule wanafunzi 14.

Queen Bey bado anaendelea na ziara yake ya ‘Formation’ huku June 28 akitarajiwa kufanya show kwenye jiji la Sunderland, Uingereza na Agosti 3 atakuwa nchini Hispania akiendelea na ziara yake kwenye jiji la Barcelona.

Hakuna maoni:
Write maoni