Timu ya taifa ya soka nchini
Ufaransa imeshinda mechi ya ufunguzi wa dimba la kombe la bara Ulaya
baada ya kuinyuka Romania, mabao 2-1, katika uwanja wa Stade de France
mjini Paris.
Dimitri Payet wa Ufaransa ambaye anaichezea klabu ya West Ham nchini Uingereza alifunga bao la ushindi katika muda wa lala salama.
Mshambuliaji wa Ufaransa Olivier Giroud alifunga bao la kwanza kwa kichwa muda mfupi tu baada ya kipindi cha pili kung'oa nanga, na baadaye Romania wakazawazisha kwa mkwaju wa penalti kutoka kwa Bogdan Stancu.
Hakuna maoni:
Write maoni